Tanzania Opposition Rejects Election Results, Calls for Fresh Poll
“The October 29 election is null and void and all results must be cancelled,” Heche said, adding that Tanzanians were denied a genuine chance to choose their leaders.
“The October 29 election is null and void and all results must be cancelled,” Heche said, adding that Tanzanians were denied a genuine chance to choose their leaders.
Opposition party Chadema’s deputy chairperson John Heche told reporters that Tanzania witnessed “mass killings of more than 2,000 people and over 5,000 injured in the space of just one week”.
Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amesema tofauti za kisiasa au mapenzi binafsi kwa kiongozi haziwezi kuwa sababu ya kuvuruga amani ya nchi, akisisitiza kuwa Tanzania imejengwa katika misingi ya demokrasia na utulivu tangu kuanzishwa kwake.
Akihutubia wazee wa Dar es Salaam leo, Rais Samia amesema kuwa Serikali ya Awamu ya Sita imeendelea kuboresha huduma za jamii na uchumi, na kwamba wanaoeneza chuki dhidi yake hawapaswi kutumia misingi ya dini au ukabila kuibua mgawanyiko.
“Hata kama aliyepo juu ya Serikali humtaki, kuna muda. Hii ni nchi ya kidemokrasia; huyu mtu ataongoza hadi kipindi hiki. Kama amefanya kosa, lisemeni kosa la kuongeza huduma bora za afya? Au kujenga mashule mazuri? Au kukuza uchumi hadi kusifiwa duniani? Kosa letu ni nini?” alihoji.
Ameongeza kuwa kutopenda kiongozi hakupaswi kuwa kichocheo cha vurugu: “Kama mtu hampendi anayeongoza, tustahimili tu. Ataongoza, ataondoka. Wote walioongoza tangu awamu ya kwanza, je, wote walipendwa? Kulikuwa na vurugu? Kama haumpendi Samia kwa sababu ya dini yake au alikotoka, hakuna sababu ya kuvuruga nchi.”
Rais Samia pia aliwaonya wananchi dhidi ya kile alichokiita “sumu za kisiasa” zinazoenezwa kwa jina la dini, akisema mbinu hizo hujenga chuki na kuharibu umoja wa taifa.
“Niwaombe sana: zile sumu zinazotiwa huko, mnapotiwa sumu tumieni akili zenu. Hakuna eneo baya la kumpata mtu kama dini; ukimlisha ubaya unajenga chuki moyoni. Wanasiasa wanamuharibu mtu kichwani,” alisema.
Katika wito mahsusi kwa viongozi wa dini, Rais Samia aliwahimiza kudumisha misingi ya maadili na kushikilia nafasi yao kama walinzi wa amani ambapo moja kwa moja alilitaja Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania(TEC), ambao mara kadhaa wamekuwa wakitoa waraka mzito dhidi ya mamlaka.Rais Samia alisema baraza hilo limekuwa likitoa matamko mara kwa mara, ikiwemo manane yaliyotolewa katika kipindi kifupi. Hata hivyo, amesema hata ndani ya TEC kuna viongozi wanaopinga matamko hayo wakiyaita batili, jambo analosema linaonesha kuwa msimamo huo si wa taasisi nzima.
“Viongozi wa dini kaeni kwenye mstari wenu. Dini zetu zote zinasema mamlaka yote yamewekwa na Mungu iwe mwanamke au mwanaume. Mungu ndiye anajua kwa nini Samia yupo hapa. Majoho yenu yaoneshe sura halisi. Hakuna kitabu cha dini kilichosema kitumie dini kuvuruga nchi,” alisisitiza.
Amehitimisha kwa kuwataka viongozi wa kidini na wananchi wote kulinda umoja wa kitaifa na kuepusha misuguano inayoweza kuhatarisha amani ya Tanzania.
Several MEPs spoke about the violent crackdown on protesters, the imprisonment of nearly all major opposition leaders and the treatment of activists from Kenya and Uganda who were beaten and tortured for observing Tundu Lissu’s trial.
Makamu Mwenyekiti wa Chadema, John Heche, akitoa taarifa kwa vyombo vya habari leo Novemba 19, 2025, amesema Rais Samia hana mamlaka ya kimaadili wala kisiasa kuunda chombo cha kuchunguza kile chama hicho kinachokitaja kuwa ni uhalifu uliotekelezwa na Serikali yake dhidi ya raia waliokuwa wakidai haki zao za kidemokrasia.
Wakili Mkuu wa Serikali Nassoro Katuga, ulieleza kwamba mapingamizi yaliyotolewa na mshtakiwa yanahitaji muda zaidi kujibiwa kwa kina, kwani yanagusa vifungu kadhaa vya sheria za ndani na za kimataifa.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Sheria na Haki za Binadamu wa CHADEMA, Wakili Gaston Garubindi, maombi hayo yamesajiliwa na kupangwa mbele ya Jaji Obadia Bwegoge.
Taarifa hiyo ya ACT Wazalendo ambayo imetolewa leo Alhamisi Novemba 6, 2025, imeeleza kuwa matukio hayo si uvunjifu wa haki za binadamu tu bali pia mamlaka zimekosa utu kwa kutozingatia misingi ya utawala bora.
Katika ripoti yake ya awali, Ujumbe wa Waangalizi wa Uchaguzi wa AU ulisema kuwa baadhi ya wapiga kura walipatiwa karatasi nyingi za kupigia kura, na wengine waliruhusiwa kupiga kura bila majina yao kuthibitishwa kwenye daftari la wapiga kura.
Idadi ndogo ya wapiga kura imeonekana katika vituo vya kupigia kura jijini Dar es Salaam leo Jumatano, wakati ambapo wapinzani wakuu wa Rais Samia Suluhu Hassan wengine wakiwa gerezani na wengine wamezuiwa kugombea.