Afrika yakabiliwa na upungufu wa dawa ya usingizi kwa upasuaji wa watoto
Halothane bado inatumika kwa kiasi kikubwa katika nchi za Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara kuwapa watoto usingizi wakati wa upasuaji. Sababu kuu ni kwamba dawa hiyo ni nafuu zaidi, ikiwa na gharama mara saba hadi kumi chini ya mbadala wake wa kisasa, sevoflurane.