Somalia yasajili wagombea 39 kwa kura za urais

Uchaguzi huo umecheleweshwa kwa mwaka mmoja na umekumbwa na ghasia mbaya na mzozo wa kuwania madaraka kati ya Rais Mohamed Abdullahi Mohamed, na Waziri Mkuu Mohamed Hussein Roble.

0
Mohamed Abdullahi Mohamed ‘Farmajoo’ Rais wa Somalia

Somalia imeandikisha rekodi ya kuwa na wagombea 39 watakaoshiriki uchaguzi wa rais utakaofanyika Mei 15. Kamati ya bunge iliyopewa jukumu la kuandaa uchaguzi umecheleweshwa kwa muda mrefu katika taifa hilo dhaifu la Pembe ya Afrika.

Uchaguzi huo umecheleweshwa kwa mwaka mmoja kulingana na ratiba, na umekumbwa na ghasia mbaya na mzozo wa kuwania madaraka kati ya Rais Mohamed Abdullahi Mohamed, anayejulikana zaidi kama Farmajo, na Waziri Mkuu Mohamed Hussein Roble.

Wabunge na maseneta watamchagua mkuu wa nchi ajaye, uchaguzi utafanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu unaolindwa vikali dhidi ya uasi wa Kiislamu uliodumu kwa muongo mmoja.

Wagombea hao ni pamoja na marais wawili wa zamani, Hassan Sheikh Mohamud (2012-2017) na Sharif Sheikh Ahmed (2009-2012) pamoja na waziri mkuu wa zamani, Hassan Ali Khaire (2017-2020).

Rais wa eneo la Puntland Said Abdullahi Dani na waziri wa zamani wa mambo ya nje ambaye pia aliwahi kuwa naibu waziri, Fawzia Yusuf Adan (2012-2014) pia ni miongoni mwa waliojiandikisha kugombea.

Mgombea atakayeshinda uchaguzi lazima apate kuungwa mkono na thuluthi mbili ya manaibu na maseneta, ikiwa ni kiwango cha chini cha kura 184.

Uchaguzi hatimaye utamaliza mzozo mrefu wa kisiasa ulioahirishwa mara kadhaa.

Baada ya muhula wa Farmajo kumalizika Februari 2021 bila uchaguzi mpya kufanyika, alijaribu kurefusha utawala wake kwa amri, na kusababisha mapigano makali ya mitaani huko Mogadishu huku makundi yanayohasimiana yakipigana.

Kufuatia shinikizo la kimataifa, alimteua Roble kutafuta makubaliano juu ya njia ya kupata mwafaka, lakini mchakato uliendelea polepole, na kuzua hofu ya kukosekana kwa utulivu nchini.

Siku ya Jumanne, washirika 30 wa kimataifa wa Somalia waliwataka viongozi wa nchi hiyo “kuhitimisha hatua hii ya mwisho ya mchakato wa uchaguzi kwa haraka, kwa amani na kwa kuaminika.”

Waliotia saini taarifa hiyo ni pamoja na Umoja wa Afrika na Umoja wa Nchi za Kiarabu pamoja na nchi za Magharibi kama vile Marekani na Uingereza.

Nchi za Kiarabu zikiwemo Qatar, Falme za Kiarabu na Saudi Arabia pamoja na Urusi na Uturuki pia zilitia saini taarifa hiyo.

In this article

East Africa Premier News Source with Top Stories, Special Features and more.
Uncensored & Undaunted